May 5, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Muonekano wa gari alililopata ajali nalokiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe wakiwemo makada wengine

Zitto, makada watano wanusurika ajalini

Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Oline, Kigoma

KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amepata ajali ya gari akiwa njiani akitokea Kata ya Kalya kuelekea Lukoma kwenye kampeni katika Jimbo la Kigoma Kusini.

Muonekano wa gari alililopata ajali nalokiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe wakiwemo makada wengine wa chama hicho

Taarifa iliyotolewa kwenye vyombo vya habari iliyotolewa na Afisa Habari ACT-Wazalendo, Arodia Peter, ilieleza kuwa ajali hiyo ilitokea jana ambapo Zitto alikuwa na watu watano kwenye gari yake.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo Zitto na watu hao ote wako salama ingawa walipata majeraha na wanahisi maumivu makali. Taarifa hiyo ilieleza kwamba baada ya ajali hiyo walipata huduma ya kwanza kwenye eneo la ajali baadaye walipelekwa Kituo cha Afya cha Kalya kilichopo Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma.

Mwisho