September 12, 2026

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

 Na Mwandishi Wetu,Dar BAADHI ya wasusi jijini Dar-es-Salaam wameiomba kampuni ya Darling Hair kupanua wigo wa programu yake ya Loyalty Program ili kuwafikia wasusi wengi zaidi, wakisema mpango huo umekuwa na manufaa kwao katika kipindi cha miaka miwili tangu kuanzishwa kwake.  Rai hiyo imetolewa katika hafla ya kutimiza miaka miwili ya programu hiyo iliyowakutanisha wasusi kutoka Kariakoo,Magomeni,Manzese na maeneo ya jirani katika ukumbi wa Sinza Deluxe, jijini Dar-es Salaam. Hafla hiyo ilihusisha michezo, muziki, vyakula, zawadi na burudani mbalimbali.  Queen Mgao,msusi kutoka Kariakoo amesema,kuongezwa kwa idadi ya wasusi wanaonufaika na programu hiyo kutawapa fursa zaidi ya  kukusanya  lebo  na  pointi ...