Esther Macha, TimesMajira Online, Kyela
MPIGAMPICHA maarufu Jijini Mbeya, Obadia Mwakibinga amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea Ubunge Jimbo la Kyela.
Mwakibinga amesema nia ya kuomba kuteuliwa ni kusaidiana na wananchi wa Kyela kuleta maendeleo.
Aidha amesema changamoto zaJjimbo la Kyela ni pamoja afya, maji, miundo mbinu ya barabara maeneo ya vijijini ni changamoto kubwa.
Akimkabidhi fomu ya kugombea Ubunge, Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Kyela, Lucas Nyanda amewataka wagombea kufuata kanuni na taratibu za chama ikiwa ni pamoja na kuacha tabia ya kujipitisha kwa wapiga kura kabla ya kampeni kuanza.

More Stories
Kigoma yatoa tenda zaidi ya Milioni 500
Vyama vya Siasa vyatakiwa kuwa Mabalozi wa Bima
Serikali kuboresha hadhi ,maslahi ya madereva