Na Joyce Kasiki, TimesMajira Online, Dodoma
MBUNGE wa Konde Khatib Said Haji (ACT-Wazalendo) amefariki alfajiri ya leo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa akipatiwa matibabu.
Akitoa taarifa leo Bungeni jijini Dodoma,Naibu Spika Dkt.Tulia Ackson amesema mwili wa mbunge huyo utazikwa leo saa kumi jioni visiwani Zanzibar.
Kufutia kifo cha Mbunge huyo Bunge limeahirishwa hadi kesho saa tatu asubuhi.

More Stories
eGA yaimarisha kilimo kupitia Mifumo ya Kidigitali
Cyber Bullying: Unyanyasaji wa Mtandaoni
Mbegu bora msingi wa mapinduzi ya kilimo nchini