Na Penina Malundo, TimesMajira Online, DSM
VIONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wameondoka Ofisi za Makao Makuu wamewasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), kumpokea Makamu Mwenyekiti wa Chama Taifa (Bara) . Tundu Lissu .
Lissu atatua uwanjani hapo saa 7.20 mchana huu. Baada ya kupokelewa JNIA, Makamu Mwenyekiti huyo ataelekea Ofisi za Makao Makuu ya Chadema, Mtaa wa Ufipa, jijini Dar es Salaam, ambako atazungumza na Waandishi wa Habari.

More Stories
eGA yaimarisha kilimo kupitia Mifumo ya Kidigitali
Mbegu bora msingi wa mapinduzi ya kilimo nchini
Waziri Mkuu Aipongeza TAFICO kwa mafanikio Nanenane