May 14, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Klopp amtaka kocha Uholanzi kumuacha Van Dijk

LIVERPOOL, England

MENEJA wa Liverpool Jurgen Klopp amemsihi kocha wa timu ya Taifa ya Uholanzi Frank de Boer kumwacha beki wa timu hiyo Virgil van Dijk, katika kikosi chake kitakachoshiriki Mashindano ya Uropa msimu huu wa kiangazi ili kumpa muda wa kutosha kupona jeraha lake la goti.

Van Dijk, mwenye umri wa miaka 29 raia wa Uholanzi, amekuwa nje ya uwanja tangu Oktoba mwaka jana, baada ya kupata jeraha la goti lakini mchezaji huyo amekuwa akifanya kazi bila kuchoka ili kupona haraka iwezekanavyo na hivi majuzi alichapisha video akikimbia bila msaada kama sehemu ya kupona.

Ishara zote zinaonyesha Van Dijk yuko njiani kupona vizuri, lakini Klopp amesisitiza kuwa mchezaji huyo anatakiwa kupunzika msimu wote wa joto ili kupata nguvu kamili na atakuwa akihatarisha kazi yake kwa kujaribu kurejea dimbani hivi karibuni.

“Hakuna mtu anayemzuia Virgil. Hakuna anayejua kwa sasa ni lini itakuwa sawa, lakini unaweza kufikiria hakika itakuwa ngumu sana na Euro kwa sababu hayuko kwenye mazoezi ya timu bado na hatakuwa katika wiki chache zijazo. Kwa hivyo sijui. Lakini mwishowe ni uamuzi wake.” amesema Klopp.

De Boer hapo awali alikiri kwamba Van Dijk atakuwa na uamuzi wa mwisho linapokuja suala la kujumuishwa kwake, akisisitiza kwamba beki wa Liverpool hana “shinikizo” la kucheza kwenye mashindano haya ya majira ya joto.

Bosi huyo wa Uholanzi anataka kikosi chake kiwasilishwe ifikapo Juni 1, na ikiwa Van Dijk amerudi kwenye mazoezi kufikia wakati huo, ni ngumu kumuona akiingia kwenye ndege msimu huu wa joto.