Na Mwandishi Wetu,Timesmajiraonline,Mara
Leo Juni 30, 2025, Mbunge aliyemaliza muda wake wa viti Maalumu Mkoa wa Mara Ghati Zephania Chomete, amechukua fomu kuomba kuteuliwa kugombea ubunge kuwakilisha wanawake kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa mkoa huo.
Ghati Chomete amekabidhiwa fomu hiyo Juni 30, 2025, makao Makuu ya CCM Mkoa yaliyopo Mjini Musoma na Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi Tanzania (UWT) Mkoa wa Mara Nderi Amos Isangya.



More Stories
RC akemea uvuvi haramu
DC:World Vision chachu ya maendeleo nchini
Usimikaji mitambo hewa tiba wamkosha Kihongosi