Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online
Katibu Mkuu wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbas amewaongoza viongozi mbalimbali wa michezo wa mataifa ya Afrika kushuhudia mashindano ya soka yanayoendelea ya bara la Afrika CANAF 2021 jijini Dar.
Katika mechi ya Timu ya Kenya na Zanzibar, Kenya imeshinda magoli 5-0 dhidi ya Zanzibar katika Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es Salaam.
Goli la kwanza na Nicholous Keiyo dakika ya 20 la pili dakika ya 23 na Mohamed Mungi la tatu dakika ya 33 na Augeni Makanga.

Goli la nne dakika ya 36 na mshambuliaji Diniel Safari wakati goli la 5 limefungwa na Albelt Mwakinga.
Hadi sasa timu ya Zanzibar ndiyo inayoongoza kwa kufungwa zaidi ikiwa imefungwa jumla ya magoli 17 wakati yenyewe haijaambulia hata goli moja.

More Stories
Wajinyakulia zawadi Kampeni ya ‘Vuna na Mixx’
Ajishindia Mil. 50 ‘Kila muamala bao la ushindi’
Watanzania zaidi ya 90 wanufaika ‘ ikiingia tu goli’