April 20, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Profesa Ibrahimu Lipumba akihutubia kwenye mkutano

Mgombea urais kwa tiketi ya CUF Profesa Ibrahim Lipumba akihutubia mamia ya wananchi wa Kata ya Ilula wilayani Kilolo mkoani Iringa ambapo aliomba kura kwa wananchi.

CUF yaahidi kuwekeza kwenye rasilimali watu

Na Hadija Bagasha,Iringa

CHAMA cha Wananchi (CUF) kimesema endapo kitapata ridhaa ya kuongoza nchi kitawekeza kwenye rasilimali watu ikiwemo afya na elimu.

Hayo yalisemwa na mgombea urais Prof. Ibrahimu Lipumba kupitia chama hicho wakati akihutubia wananchi wa Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa ambapo alisema kama watu hawana elimu na afya bora ukiwekeza kwenye vitu haitawasaidia chochote.

Mgombea urais kwa tiketi ya CUF Profesa Ibrahim Lipumba akihutubia mamia ya wananchi wa Kata ya Ilula wilayani Kilolo mkoani.Picha zote na Hadija Bagasha Iringa.

Lipumba alisema Serikali ya CCM imekuwa ikiwekeza kwenye kununua vitu kama vile ndege badala ya kuwekeza kwenye miundombinu muhimu ya afya na elimu.

‘Endapo tutapewa ridhaa Sera ya CUF itawekeza kwenye vitu muhimu vya afya na elimu ili viweze kuja kuwasaidia watanzania katika kujikwamua na umaskini.,”

Kama Taifa lazima tuwe na utaratibu wa kuhakikisha watoto wanapata lishe bora ili kujikengea kinga ya mwili na Serikali ina kila sababu ya kuhakikisha wanapata elimu bora.

Profesa Lipumba alisema muungano ni muhimu na endapo watachaguliwa wataimarisha muungano kati ya Tanzania bara na Zanzibar na kuwa na haki sawa kwa pande zote mbili.

Alisema watakapopata ridhaa hiyo ya kuongoza nchi wataendeleza muungano kwa kuwa ni muhimu kwa Taifa letu.

Mgombea mwenza Hamida Abdalah Huweish akihutubia wananchi wa Kilolo Mkoani Iringa.

Katika hatua nyingine mgombea urais huyo alisema Serikali ya CCM imeiacha solemba sekta ya kilimo na bila mapinduzi ya kilimo hawawezi kuleta mapinduzi ya viwanda hivyo CUF inahitaji kuleta mabadiliko na mapinduzi katika sekta hiyo.

Alisema wanahitaji kuleta mabadiliko ili pawepo na mzunguko wa fedha kwani wananchi wa Kilolo ni watu wanaojishughulisha na kilimo lakini hawana msaada wowote wowote wanaoupata kutoka serikalini.

Tunaomba kura zenu ili biashara zitoke na wananchi waweze kufanya biashara uwekezaji uongezeke vitunguu vipate soko sio tu Tanzania mpaka Africa mashariki yote watu wapewe utaalamu wa kuweza kuongeza tija katika shuhjuli zao za kilimo…wapate zana na kuweza kumwagilia na za kilimo.

Hata hivyo alisema kuwa unapoongeza tija kwenye kilimo ndipo unapopata uwezo wa kuendeleza viwanda kwani kilimo kinatoa chakula na endapo kilimo kikiwa na tija uzalishaji utaongezeka.

Baadhi ya viongozi wa CUF wakiimba wimbo wa chama hicho

Kwa upande wake mgombea mwenza Hamida Abdalah Huweishi amewataka vijana wasijutie kuzaliwa kwani muda uliopita siyo muafaka kwani cuf itawaboresha katika kila aina ya sekta kwa kutumia rasilimali za nchi zilizopo.

Vijana siyo taifa la kesho ni Taifa la leo Sera ya Taifa la kesho ipo CCM na imewaweka kwenye uongo mtupu na kuacha rushwa itawale pigeni kura CUF ili muyaone mabadaliko hamkuzaliwa kuja kuongeza idadi ya makaburi CUF imedhamiria kuwainua,’alisema Mgombea.