Na Mwandishi wetu,Timesmajira Airtel Tanzania imeendelea kuimarisha mahusiano na ushirikiano wa kimkakati na wateja kupitia mashindano ya Airtel Business Monthly Mug Tournament yaliyofanyika katika Klabu ya Gymkhana jijini Arusha, Tanzania. Mashindano hayo yaliwaleta pamoja viongozi wa biashara, wateja, na wadau mbalimbali, yakitoa fursa ya kujenga mahusiano yenye tija, kubadilishana mawazo, na kutambua fursa mpya za ukuaji wa biashara nje ya mazingira ya kawaida ya kikazi sambamba na kutambua na kuunga mkono mchezo wa Gofu nchini. Akizungumza wakati wa mashindano hayo, Mkurugenzi wa Airtel Business, Joseph Vipond, amesema Airtel inaamini ushirikiano imara hujengwa kupitia mawasiliano ya karibu na ushiriki endelevu, huku michezo ikitoa jukwaa bora la kuimarisha mahusiano hayo. Kwa upande wake, Meneja wa Mahusiano kwa Umma wa Airtel Tanzania, Sarah Nassor, amesema mashindano hayo yanaonyesha dhamira ya kampuni ya kujenga uhusiano wa kudumu na wadau kwa kuwashirikisha katika masuala yanayochochea mawasiliano, uaminifu, na ushirikiano katika nyanja mbalimbali. Moja wa watumiaji wa huduma za Airtel ,Hiten Nathwani, ameipongeza kampuni ya Airtel kwa kuendelea kuboresha huduma zake sambamba na kuwasihi wachezaji Gofu hao kutumia huduma za Airtel.  Kupitia Airtel Business Monthly Mug Tournament, Airtel Tanzania inaendelea kuonyesha kuwa ushirikiano wenye tija hujengwa zaidi ya mahusiano ya biashara kwa kuunganisha watu toka sehemu mbalimbali na kuunganisha jamii ili kuchochea ukuaji endelevu wa uchumi jumuishi wa kidijitali nchini.
Penina Malundo
Na Mwandishi wetu,Timesmajira Kampuni ya GF Vehicle Assemblers imeeleza dhamira yake ya kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kukuza...
Na Mwandishi wetu,Timesmajira Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Hamza S. Johari, amekitaka Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) kuwa wabunifu na...
Na Penina Malundo,Timesmajira Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Africa50 pamoja na Jukwaa la Miundombinu Afrika (Infra for Africa...
Na.Mwandishi wetu,Timesmajira Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), inaendelea na utekelezaji wa Mkakati mkubwa wa kuimarisha kilimo cha...
Na.Mwandishi wetu,Timesmajira Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya...
Na Penina Malundo,Timesmajira Tanzania itakuwa mwenyeji wa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Africa50 (General Shareholders' Meeting - GSM) pamoja na...
Na Mwandishi Wetu,Timesmajira NAIBU Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, James Millya, ameutaka uongozi na wataalamu...
Na Mwandishi wetu,Timesmajira MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeendelea kutoa elimu kwa wananchi wanaotembelea banda lake katika Maonesho ya Nanenane...
Na Mwandishi wetu,Timesmajira Wakala wa Vipimo (WMA) imetoa elimu kwa wajasiriamali wanaoshiriki Maonesho ya Nane Nane Kitaifa yanayofanyika katika Viwanja...
