April 18, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Umoja wa Ulaya wajadili siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia

Na David John

MkUU wa ujumbe wa Umoja wa Ulaya Manfreo Fanti akiwa pamoja na mabalozi wa Nchi wanachama wa Eu Nabil Hajlaoui ambaye ni balozi wa ufaransa nchini na wengine wamekutana na waandishi wa habari na kuzungumzia siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.

Akizungumza katika mkutano huo mbele ya vyombo vya habari uliofanyika katika kituo cha utamaduni cha ufaransa Fanti alisema wamefanya mkutano huo kuwasilisha mpango wa mwaka huu kuhusu siku 16 za kupinga Ukatili wa Kijinsia nchini Tanzania.

Amesema kuwa siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia ni kampeni ya kimataifa inayolenga kuongeza uelewa kuhusu athari za ukatili, hasa kwa wanawake na wasichana wadogo.

“kampeni hii inasisitiza kwamba unyanyasaji dhidi ya wanawake, kwa namna yoyote, ni ukiukwaji wa
haki za binadamu na Kwamba wanawake wote, wasichana, wanaume na wavulana katika utofauti wao wote – wanapaswa kuchukua msimamo dhidi yake.

Nakuongeza “Hapa ni Nchi Wanachama wa EU zimeungana na UNFPA na washirika wamejitolea kukomesha unyanyasaji wa kijinsia.

Amesema Katika siku 16 za mwaka huu za uharakati balozi za Ubelgiji, Denmark, Finland, Ufaransa, Ujerumani, Ireland,
Uholanzi, Uhispania, Uswidi na Ujumbe wa EU pamoja na wadau wa kitaifa na UNFPA watapanga matukio kadhaa ya umma jijini Dar es Salaam na mkoa wake kuanzia Novemba 25 hadi Desemba 10 ,2021.

Fanti ameongeza kuwa Maadhimisho hayo yatahitimishwa kwa tuzo ya Bingwa wa Pamoja wa UWAKI na tamasha la kukusanya fedha kuandaliwa.na timu ya Ulaya, Muungano wa MKUKI, WiLDAF pamoja na UNFPA.

Amefafanua kuwa tukio hilo litafanyika Jumatano Desemba 8,2021, kuanzia saa 19:00 Jioni katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam na maonyesho ya watu mashuhuri wa kitaifa Akiwamo Ben Pol, Nandy, Siti na Bendi, Muziki wa Bedja na Shikandol .

Naye Balozi wa ufaransa Hajlaoui akizungumzia siku 16 kupinga ukatili wa kijinsia hususani Tanzania amesema ni muhimu kuendelea kuwainua wanakwake na kuondoa mfumo dume ili kuwa sawa na ameshauri nivema kuepukana na hilo ili kuleta usawa.

Hajlouoi ameongeza kuwa lazima elimu iendelee kutolewa hata kwa kupitia siasa na bahati nzuri Tanzania inaongozwa na rais mwanamke na kwamba kwa ufaransa ukatili wa kijinsia upo kwenye upande wa elimu lakini wanajalibu kutafuta ufumbuzi na wanapiga hatua kubwa.

Mkuu wa ujumbe wa umoja wa ulaya Manfredo Fanti pamoja na mabalozi wanaowakikisha nchi zao Tanzania ambao ni wanachama wa umoja huo EU wakiwa katika tukio maalum mbele ya waandishi wa habari hawapo pichani .wakizungumzia siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
Mabalozi mbalimbali wa umoja wa ulaya Eu wanaowakilisha nchi zao hapa nchini akiwamo balozi wa ufaransa Nabil Hajlaoui wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mkutano na waandishi wa habari uliozungumzia namna ya kukabiliana na ukatili wa kijinsia

Bolozi wa Ireland hapa nchini Ms Mary O’Neill ku akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu siku 16 za kupinga na utoaji elimu ya kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsi ambapo kilele chake Desemba 8 mwaka huu wa pili kushoto ni NabilHajloui balozi wa ufaransa nchini na watatu kushoto ni Mkuu wa ujumbe wa umoja wa ulaya Manfredo Fanti.