April 26, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dkt. Edwin Mhede akizungumzia mafanikio ya TRA katika kipindi cha miaka mitano ya Serikali ya Awamu ya Tano wakati wa uzinduzi wa kikao kazi cha tathmini ya utendaji kazi wa Idara ya Kodi za Ndani kinachofanyika mkoani Mbeya na kitahitimishwa Septemba 6,mwaka huu.Picha na Veronica Kazimoto

TRA yaongeza makusanyo yafikia trilioni 17.87

Na Esther Macha,Timesmajira,Online , Mbeya

KAMISHNA Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dkt.Edwin Mhede amesema kuwa mamlaka hiyo imefanikiwa kuongeza ukusanyaji wa mapato  kutoka mwaka 2014/2015 na kuongezeka  kutoka trilion 10.67 mpaka kufikia trilioni 17.87 katika mwaka wa fedha 2019/2020.

Amesema kuwa katika kipindi cha miaka mitano wameweza kuongeza ukusanyaji wa mapato  na kuiwezesha serikali kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo  pamoja na huduma za kijamii.

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dkt. Edwin Mhede akizungumzia mafanikio ya TRA katika kipindi cha miaka mitano ya Serikali ya Awamu ya Tano wakati wa uzinduzi wa kikao kazi cha tathmini ya utendaji kazi wa Idara ya Kodi za Ndani kinachofanyika mkoani Mbeya na kitahitimishwa Septemba 6,mwaka huu.Picha na Veronica Kazimoto

Dkt.Mhede amesema hayo jana wakati wa ufunguzi  wa kikao  kazi cha tathmini utendaji kazi  wa  idara ya kodi za  ndani  kikao hicho cha siku nne(4)kinachofanyika katika ukumbi wa NHF Jijini Mbeya  ambacho kimeshirikisha Mameneja wa Mikoa yote 30 ya kikodi ya Tanzania Bara,na mameneja wasaidizi .

Aidha Kamshina Mkuu huyo amesema kwamba makusanyo hayo ni ongozeko la wastani wa kutoka Bilion. 850 zilizokuwa zinakusanywa kwa mwezi wakati serikali ya awamu hii inaingia madarakani hadi kufikia wastani wa, trillion 1.5 kwa mwezi  ikiwa  ongozeko la asilimia 76 kwa mwezi.

Akielezea ogozeko hilo Dkt. Mhede amesema kuwa  makusanyo hayo  yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na jitihaa za hati za Serikali ya Awamu ya Tano  inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli .

Amesema kwamba TRA imekuwa ikipewa ushirikiano ikiwa ni pamoja na kuiongezea uwezo wa kiutendaji kwa kuboresha sheria na mifumo ya usimamizi wa kodi ,kudhibiti nidhamu na uadilifu katika kuzuia  mianya ya ukwepaji  kodi  kwa ujumla.

Akifungua kikao kikazi hicho Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert  Chalamila alisema mafanikio makubwa yanayokuwepo kati ya TRA na Serikali na vyombo ya dola yanafanya kuwepo na moyo wa  kulipa kodi kwa wananchi na kwamba  kuweza kufakiwa kwa kiasi kikubwa .

Aidha amesema ukweli ni kwamba uadilifu unatakiwa katika chombo hiki nakwamba wakati fulani kukiwa na mkwama wakati wa makusanyo ya kodi   huwa kunasababishwa na kukosekana na uaminifu na kuwa mara nyingi kukiwa na madili mengi suala la ukusanyaji kodi lazima liwe hafifu .

Akizungumzia utoaji wa elimu kwa walipa kodi Kaimu  Kamshna wa Idara ya kodi za ndani  (TRA),Abdul  Mapembe amesema kuwa mara nyingi wakiitisha semina wanaokuja ni wale ambao  hawahusiki sio na wakiulizwa wahusika husema wanakuwa na kazi nyingi .

“Kwa hiyo imekuwa ni mpaka wafuatwe mmoja mmoja na kumfuata mmoja ni kazi ndo maana tuna vipindi kwenye Tv na radio lakini idara hii ina watu wanazunguka Tanzania nzima  kwa hiyo elimu tunatoa sana kwa walipa kodi wetu na kuwa elimu wanayo ya kutosha”amesema Kaimu Kamishna huyo.

 Mwisho.