Na Mwandishi wetu,Timesmajira
Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) imeshiriki na kushinda tuzo ya Ubora katika Uhamasishaji Biashara ya Kimataifa na Ushirikiano wa Uchumi.
Tuzo hizo za sekta ya Umma zinaangazia ubunifu unaofanywa na taasisi mbalimbali za umma kwa muktadha wa kutoa huduma bora zinazoakisi maendeleo endelevu ya uchumi wa Tanzania.
TanTrade imekua ikifanikisha hayo kupitia Maonesho ya Sabasaba, kuratibu Maonesho mbalimbali ya Kimataifa kama vile Expo’s, Mifumo mbalimbali ya Kidigitali ya Biashara kama vile Trade Portal, Biashara App.
Hafla ya tuzo hizo zimefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.

More Stories
Maboresho sheria yaongeza ushiriki wa watanzania kwenye migodi
Wizara ya Afya yatoa elimu elekezi huduma za afya
Prof.Kabudi:Tumepiga hatua utoaji huduma za Afya