May 21, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli

Rais Magufuli asamehe wafungwa 3,973

Na Mwandishi Wetu

KATIKA kuadhimisha miaka 56 ya Muungano, Rais John Magufuli ametoa msamaha kwa wafungwa 3,973.

Kati ya wafungwa hao, 3,717 wamesamehewa vifungo vyao, na wafungwa 256 waliokuwa wanakabiliwa na adhabu ya kunyongwa hadi kufa wamebadilishiwa adhabu hiyo.

Kupitia salamu zake za maadhimisho ya Muungano, Rais Magufuli amesema ana matumaini kuwa wafungwa hao wamejifunza na watajirekebisha ili waungane na jamii katika kulitumikia Taifa wakiwa raia wema wanaozingatia sheria na taratibu.