April 24, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya Ulrich Matei

BREAKING NEWS: Aliyemuua Bibi yake na kuondoka na kichwa akamatwa

Na Esther Macha, Mbeya

HATIMAYE Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya kwa kushirikiana na wananchi wa Kiwira Wilaya ya Rungwe wamefanikiwa kumtia nguvuni kijana Eliakim James (20) kwa tuhuma za kumuua bibi yake Junes Sankanye(65) na kisha kutokomea na kichwa chake.

Kitendo hicho kilipelekea familia kulazimika kuzika kiwiliwili bila kichwa baada ya kumtafuta mtuhumiwa na kichwa cha marehemu siku mbili bila mafanikio.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Nkunga Mariam Bachu Nurdin alieleza mkasa mzima wa tukio hilo la mtuhumiwa wa mauaji kukamatwa na kichwa hicho na kuleta simanzi kubwa katika Kijiji hicho.

Kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya Ulrich Matei alithibitisha kukamatwa kwa kijana huyo ambaye ametafutwa kwa siku mbili tangu afanye mauaji hayo.

Habari kamili ipo katika gazeti la Majira …