May 10, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

PSC yapokea malalamiko ya kiutumishi

Maafisa wa Tume ya Utumishi wa Umma (kutoka kushoto) Bw. Robert Lwanji, Bw. Lamech Mapunda na Bw. Justine Jackson wakisoma vielelezo mbalimbali vilivyowasilishwa na mdau wa tume (kulia). Maafisa wa Tume walikuwa Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani kishughulikia kero na malalamiko kutoka kwa watumishi wa umma, katika Kuadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma, mwaka 2021. (Picha na PSC).
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bwana Nyakimura Muhoji (kulia) akisoma nyaraka mbalimbali zilizowasilishwa na watumishi wa umma na wadau kuhusu kero na malalamiko ya kiutumishi, baada ya kuwatembelea Maafisa wa Tume waliokuwa wakipokea changamoto za kiutendaji za watumishi Wilaya ya Kisarawe, Pwani wakati huu wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma pamoja nae ni Maafisa wa Tume Bw. Robert Lwanji (kushoto) na Bibi Florence Kazuva (Picha na PSC).
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma Bwana Nyakimura Muhoji (aliyevaa shati katikati) katika picha ya pamoja na Maafisa wa Tume walioshiriki katika kupokea na kusikiliza kero, malalamiko na changamoto za kiutendaji kutoka kwa watumishi wa umma na wadau Wilaya ya Kisarawe-Pwani  tarehe 16-18 Juni 2021 katika kuadhimisha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2021. (picha na PSC).