May 1, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Mtendaji Ilemela,atakiwa kutumia pikipiki kwa lengo kusudiwa

Judith Ferdinand,TimesMajira Online, MwanzaMtendaji wa Kata ya Ilemela, wilayani Ilemela mkoani Mwanza ametakiwa kutumia pikipiki iliyotolewa na serikali kwa lengo lililokusudiwa.

Mtendaji wa Kata ya Ilemela Nkuba Charles,akiwa juu ya pikipiki mara baada ya kukabidhiwa naMeya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Renatus Mulunga,kulia

Pikipiki hiyo ni miongoni mwa pikipiki 916 zilizotolewa Rais Samia Suluhu Hassan kwa Watendaji wa Kata nchini ambapo Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela ni moja ya wanufaika.

Hayo yamebainishwa Machi 7, mwaka huu na Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Renatus Mulunga,wakati akimkabidhi pikipiki hiyo Mtendaji huyo wa Kata ya Ilemela ambapo halmashauri hiyo imepata pikipiki moja kati ya zilizotolewa na Rais.

Mulunga, ameeleza kuwa Mtendaji huyo anapaswa kutumia pikipiki hiyo kwa lengo lililokusudiwa pamoja na kuhakikisha anatekeleza majukumu yake ipasavyo.

Kwa upande wake Mtendaji wa kata ya Ilemela Nkuba Charles, ameeleza kuwa pikipiki hiyo itamrahisishia utekelezaji wa majukumu yake ikiwemo ukusanyaji wa mapato.

Hivyo kuboresha utendaji kazi katika kata yake ya Ilemela pamoja na urahisi wa kuhudumia wananchi huku akiahidi utendaji uliotukuka kwa kuhakikisha kuwa wananchi wa kata hiyo wanapata huduma iliyo bora.

Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Renatus Mulunga,kulia akiwa ameshika a mkono na Mtendaji wa Kata ya Ilemela Nkuba Charles,ikiwa ni ishara ya kumkabidhi pikipiki Mtendaji huyo.