MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Mbarali kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali na Diwani wa kata ya Chimala mwaka 2015 hadi 2020 ,Francis Mtega amechukua fomu ya kuwania Jimbo hilo katika uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28 mwaka huu.
Mtega amekabidhiwa fomu hiyo na msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Mbarali ,Kivuma Msangi .
Mgombea huyo aliongozana na Mbunge aliyemaliza muda wake, Haroon Pilmohamed Mullar, Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi, walioteuliwa kugombea Udiwani kwenye kata kupitia Chama Cha Mapinduzi pamoja na wale waliokuwa wametia nia kuomba kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi katika nafasi ya Ubunge.
More Stories
Mwenyekiti NSSF afungua mkutano baraza la wafanyakazi
Wavamia msitu wa hifadhi na kufanya mauaji Kilosa
Rais Dkt.Samia mgeni rasmi maadhimisho miaka 85 ya TAG