Na Penina Malundo,TimesMajira ,Online
ALIYEKUWA Mbunge wa Jimbo la Kigamboni Dkt.Faustine Ndugulile amechukua fomu leo ya kutetea nafasi yake kwa mara ya tatu ya ubunge.
Hatua hiyo imekuja baada ya jana kuteuliwa na Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM TAIFA kumptisha rasmi kuwa mgombea ubunge jimbo la Kigamboni kupitia tiketi ya Chama hicho.
Dkt.Ndugulile amechukua fomu hiyo katika Ofisi ya Mkurugenzi wa wilaya ya Kigamboni leo majira ya mchana.

More Stories
Yas yazindua Mnara wa 5G Masasi
Wafanyabiashara wahimizwa kutumia nembo ya Tanzania
Tozo ya mafuta yaboresha barabara Mwanza