Na Penina Malundo,TimesMajira ,Online
ALIYEKUWA Mbunge wa Jimbo la Kigamboni Dkt.Faustine Ndugulile amechukua fomu leo ya kutetea nafasi yake kwa mara ya tatu ya ubunge.
Hatua hiyo imekuja baada ya jana kuteuliwa na Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM TAIFA kumptisha rasmi kuwa mgombea ubunge jimbo la Kigamboni kupitia tiketi ya Chama hicho.
Dkt.Ndugulile amechukua fomu hiyo katika Ofisi ya Mkurugenzi wa wilaya ya Kigamboni leo majira ya mchana.

More Stories
Kapinga amwezesha mwenye ulemavu Mashine kusaga viungo
Dkt.Latifa:Sabasaba yafungua milango ya masoko ya Kimataifa
TCAA yaimarisha dawati huduma kwa Wateja