Na Mwandishi Wetu, TimesMajira ONline

MWENYEKITI wa Chama cha ACT-Wazalengo, Maalim Seif Sharif Hamad leo amechukua fomu ya kugombea nafasi ya Urais visiwani Zanzibar kupitia chama hicho katika uchaguzi mkuu wa Viongozi utakaofanyika Oktoba mwaka huu.
Maalim Seif amekabidhiwa fomu hiyo leo na Katibu Mkuu wa ACT- Wazalendo, Ado Shaibu katika ofisi za Chama za Vuga Zanzibar.
Itakumbukwa kuwa, hivi karibuni baadhi ya wanachama wa chama hicho walijitokeza na kumabidhi kiongozi huyo fedha walizomchangia wakitaka azitumie kwa ajili ya kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo.

More Stories
Serikali:Usimamizi madhubuti wapunguza udanganyifu mitihani
Hafla uzinduzi Mji wa Serikali yaahirishwa
Samizi ataka NHIF kuongeza kasi usajili wanachama