April 20, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Djokovic anyakuwa ubingwa wa tenis Wimbledon

LONDON, England

NYOTA nambari moja ulimwenguni katika mchezo wa tenis

kwa upande wa wanaume Novak Djokovic, amefanikiwa

kunyakuwa ubingwa wa tenis katika mashndano ya Wimbledon

kwenye mchezo wa fainali uliofanyika mwishoni mwa wiki

nchini Uingereza.

Djokovic, mwenye umri wa miaka 34 raia wa Serbia ameweka

rekodi ya Grand Slam ya 20 kwa kuibuka na ushindi wa

seti 6-7 (4/7), 6-4, 6-4, 6-3 dhidi ya slugger Matteo

Berrettin raia wa Italia.

Akizungumza mara baada ya mchezo huo Djokovic

amesema,amefurahi sana kunyakuwa taji la Wimbledon huku

ikiwa Grand Slam yake ya 20, kwani alicheza sana vizuri

katika fainali hiyo.

Djokovic,

ambaye alikuwa akicheza fainali yake ya 30

kwenye Slams, aliongeza

bada ya kunyakuwa Australia

Open, Roland Garros

na na US Open.