April 26, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Antetokounmpo apiga alama 41 kuiua Suns game ya 3

MILWAUKEE, Washington

NYOTA wa kikapu katika timu ya Milwaukee Bucks, Giannis Antetokounmpo ameisaidia timu yake kuibuka na ushindi katika mchezo wa fainali game ya 3, Ligi Kuu ya Kikapu nchini Marekani NBA uliofanyika mwishoni mwa wiki huko Milwaukee.

Katika mchezo huo, Antetokounmpo aliifungia timu yake alama 41 na kuwafanya Bucke kuibuka na ushindi wa vikapu 120-100 dhidi ya Phoenix

Suns katika Mchezo 3. Hata hivyo Suns wanaongoza

2-1, na Mchezo 4 utafanyika kesho.

Akizungumza mara baada ya mchezo huo kumalizika kocha wa Suns Monty Williams amesema, robo ya pili na ya tatu kikosi chake hakikucheza vizuri.

Hata hivyo, Suns ilikuwa na wachezaji watano katika takwimu mbili, wakiongozwa na

Pointi 19 za Chris Paul. Deandre Ayton alikuwa na alama 18 na

rebound tisa. Jae Crowder pia alikuwa na alama 18.

%%%%%%%%%%%%%%%%