LONDON, England
KLABU ya Arsenal imemsajili beki wa kikosi cha vijana
timu ya taifa ya Ureno U21, Nuno Tavares kutoka
Benfica.
Mchezaji huyo, mwenye umri wa miaka 21, ambaye ni
usajili wa kwanza wa Arsenal msimu huu wa joto katika
makubaliano, wenye thamani ya pauni milioni 8,
Tavares, atajiunga na wachezaji wenzake huko kaskazini
mwa London mara tu atakapomaliza kipindi chake cha
kukaa Karantini.
Hata hivyo, Tavares ni zao la timu ya vijana ya Benfica
na amecheza jumla ya mechi 25 kwa klabu tangu
alipocheza kikosi cha kwanza kwenye Kombe la Super Cup
la Ureno dhidi ya Sporting Lisbon mnamo Agosti 2019.

More Stories
Yas yaendelea kuunga mkono Selous Marathon
Mwinjuma aongoza maelfu washiriki mbio TCB Selous Marathon
Mabalozi wasafiri kwa SGR kushiriki Grand Bunge Bonanza