April 25, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Wasanii waguswa na ajali ya Moto soko la Kariakoo, Marogoro

Na Mwandishi Wetu, Timesmajira Online

WASANII mbalimbali hapa nchini wameguswa vikali na

ajali ya moto iliyotokea usiku wa kuamkia leo kwenye

Soko Kuu la Kariakoo jijini, Dar es Salaam na ile ya

Bweni la Shule ya Sekondari ya Kiislam ya Wasichana AT

-TAUN inayomilikiwa na Taasisi ya Kiislam iliyopo mji

Mpya katika Manispaa ya Morogoro.

Wakitoa pole kwa waliokumbwa na mahafa hayo, kupitia

kwenye Kurasa zao za Instagrama wasanii hao wamesema

kutokana na matukio hayo mamlaka husika zitafanya kazi

yake ili kubaini chanzo.

Nandy

MSANII wa muziki wa Bongo fleva ambaye kwa sasa

anafanya vizuri katika Festival yake Faustine Charles

maarufu kama ‘Nandy’amewapa pole nyingi sana wafanya

biashara wote wa soko la Kariakoo kutokana na hali

iliyowakuta

“Moyo wa uvumilivu na subira viwe juu yetu. Hili janga

na Taifa Mungu Ibariki Tanzania,” ameandika Nandy

kupitia kwenye Ukurasa wake wa Instagram.

Shilole

Naye msanii wa muziki wa Bongo fleva na Mjasiriamali

hapa nchini Zuwena Mohamed maarufu kama ‘Shilole’

amejawa na huzuni kufuatia wajasiriamali wenzake

waliopo sokoni Kariakoo kupatwa na mahafa.

“Natoa pole kwa wajasiriamali wenzangu wote

walioharibikiwa ama kupotelewa na mali zao sokoni

kariakoo, kutokana na moto uliotokea usiku wa kuamkia

jana. Naamini mamlaka husika inafanya kazi kubaini

chanzo, ili kuweka tahadhari madhira haya yasije

kutupata tena siku za mbeleni,” ameandika shilole.

Diamondplatnumz

Kwa Upande wake, Nyota wa Bongo fleva na Bosi wa Wasafi

Media Diamondplatnumz ameguswa na ajali ya Moto ambazo

zimetokea usiku wa kuamkia jana, Moja ikiwa ya Soko la

Kariakoo na ya Pili ikiwa Shule ya Sekondari ya Kiislam

Wasichana AT -TAUN inayomilikiwa na Taasisi ya Kiislam

iliyopo mji Mpya katika Manispaa ya Morogoro.

Akizungumza kwa masikitiko kupitia kwenye Ukurasa wake

wa Instagram Diamond amesema, amepokea kwa masikitiko

makubwa kufuata kutokea kwa ajali hizo.

“Nimepokea kwa masikitiko Makubwa, ajali ya Moto

iliyotokea Morogoro na Sokoni Kariakoo.Mwenyezi Mungu

awatie nguvu Wafanyabiashara wote,pamoja na kila

aliyeguswa na ajali hii ya Moto, Mimi kama kijana wa

Kitanzania niko tayari kushiriki kwa hali na Mali

katika kurejesha faraja za ndugu zetu waliopatwa na

matatizo,” amesema Diamond.

Rosa Ree

MSANII wa muziki wa rap kwa upande wa wanawake Rosa Ree

naye ni miongoni mwa wasanii waliohudhunika na ajali ya

moto Sokoni Kariakoo iliyotokea usiku wa kuamkia jana

na ile ya Sule ya Kiislamu Morogoro.

“Mungu wangu, tunajua kwamba vyote vinavyotokea hua

sambamba na mipango yako. Basi waangalie hawa waja

wako. Watete hawa wanao Mungu wetu dah?.Poleni sana

ndugu zangu mliothirika na moto wa Kariakoo. Mungu

awape nguvu maana yake kila kitu kinawezekana,”

ameandika Rosa Ree.

%%%%%%%%%%%%%%%%%%%%%