Na Judith Ferdinand, Timesmajira Online- Mwanza
VIONGOZI 19 wa soko la Kiloleli na Mwaloni Kirumba wilayani Ilemela mkoani Mwanza waliochaguliwa hivi karibuni,wamekula kiapo cha uadilifu ili kuongoza masoko hayo kwa kipindi cha miaka mitatu wakiwemo Wenyeviti, Makatibu na Wahasibu.
Akiongoza kiapo hicho Juni 2,2026,Mwanasheria wa Serikali Wakili Kanisia Ngutu, aliwataka viongozi hao kufuata sheria , kanuni na taratibu katika kuongoza na kutatua changamoto za wafanyabiashara.

Amesema viongozi hao ni kiungo kati ya wafanyabiashara na Serikali hivyo aliwataka kulinda na kutii kiapo walichoapa kwani kwenda kinyume ni kuvunja sheria na hatua zitachukuliwa dhidi yao.
Mkuu wa Divisheni ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela,Kefa Gembe,amewataka viongozi hao viongozi kuwa daraja zuri ili kuhakikisha wafanyabiashara wanafanya shughuli za uzalishaji mali  kwa amani ili halmashauri iweze mapato ambayo yatatumika kuwaletea wananchi maendeleo.
Mwenyekiti soko la Mwaloni Kirumba Fikiri Mzinza,ameishukuru Serikali kwa miongozo na maelekezo waliowapatia na kuahidi kwenda kuwa kiunganishi sahihi kwa wafanyabiashara.
Huku Mwenyekiti soko la Kiloleli Mashimba Mabula,ameomba ushirikiano uliopo kati ya Serikali na wafanyabiashara uendelee ili kukuza biashara,mazingira mazuri na kuimarisha uchumi wa wananchi.


More Stories
Milioni 299 kutumika kujenga ofisi za kata
Mtanda asisitiza matumizi ya takwimu serikalini
Maofisa Habari watakiwa kuhabarisha taarifa sahihi