Na Mwandishi wetu,TimesMajira,Online
MGOMBEA Udiwani Kata ya Kunduchi kupitia Chama cha Mapinduzi(CCM),Michael Urio amerudisha fomu huku akiwashukuru Viongozi wa Chama cha Mapinduzi kwa kumuamini kwa mara nyingine.
Akiwa ameongozana na Wanachama wa Chama hicho wakati akirudisha fomu hiyo,amewashukuru na kuwaomba ushirikiano katika kuhakikisha wanapeperusha vema bendera ya Chama hicho.
Urio amesema kuwa kwa kushirikiana na chama chake atahakikisha anasimamia kikamilifu amani na mshikamano katika kipindi chote cha kampeni.

More Stories
Silinde azindua baraza la sita la Wafanyakazi Tume ya Taifa ya Umwagiliaji
NMB ilivyosaidia Serikali kukusanya zaidi ya Sh trilioni 9.8
Serikali yaongeza nguvu kwa wachimbaji wadogo,yasisitiza usalama Migodini