March 29, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Sherehe za miaka 57 ya Mapinduzi Zanzibar

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia suluhu Hassan, akizungumza jambo  na Rais Mstaafu wa Zanzibar Mhe. Aman Abeid Karume kwenye maadhimisho ya miaka 57 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yaliyofanyika leo Januari 12,2021 katika Viwanja vya Mnazi mmoja Mjini zanzibar. (Picha na Ikulu).
Vijana wakiwa wamebeba picha za viongozi wa sasa na wastaafu kwaupande wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Januari 12, 2021.
Zimamoto wakionyesha umahiri wao katika sherehe hizo.
Vikosi vya ulinzi na usalama vikionyesha umahiri wao.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia suluhu Hassan, akisalimiana na kuzungumza na Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad kwenye Maadhimisho ya miaka 57 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yaliyofanyika leo Januari 12,2021 katika Viwanja vya Mnazi mmoja Mjini Zanzibar.
Askari wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama, Wananchi na Wanachama wa Vyama mbalimbali vya Siasa wakiwa katika maandamano ya maadhimisho ya muaka 57 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar  yaliyofanyika Januari 12,2021 katika Viwanja vya Mnazi mmoja Mjini Zanzibar.