Na Mwandishi Wetu
Msanii wa filamu za Bongo na Mjasiriamali hapa nchini, Shamsa Ford ametoa ujumbe mzito kwa wanawake wanaopenda kuwaonga wanaume.
Akitoa ujumbe huo kupitia kwenye ukurasa wake instagram, Shamsa amesema siku zote mwanaume ukimuonga pesa jua kuna sehemu anapeleka.
“Kuna kusaidiana kwenye mapenzi na kuhonga. Hapa nazungumzia wanawake wanaowahonga wanaume pesa ili wapendwe.
“Mfundishe mwanaume wako jinsi ya kutafuta pesa na si kumuhonga. Mwanaume unayemuhonga pesa kuna sehemu na yeye anapeleka ili aonekane kidume,” amesema Shamsa.
More Stories
Twanga Pepeta waikubali ‘Speed’ ya Rais Samia
Ali Kiba aitaka jamii kuwasaidia watoto wenye uhitaji maalumu
Azam TV yazindua filamu mpya