April 27, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Rais wa Chama cha Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Matibabu ya Fistula aongoza timu ya wataalamu mabingwa wa fani hiyo

Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online

Rais wa Chama cha Madaktari Bingwa wa Upasuaji wa Matibabu ya Fistula Dkt. James Chapa (Kulia kwa Mhe Waziri) ameongoza timu ya wataalamu mabingwa wa fani hiyo akiwemo Dkt. Mtinangi na Dkt. Haule kuonana na Waziri wa Afya kujitambulisha na kuomba ushirikiano katika kuwezesha programu ya matibabu ya Fistula inayotekelezwa na Chama hicho kwa ushirikiano na Wizara ya Afya na wataalamu toka nje ya nchi MMS Foundation Canada ambao Septemba 2021 waliweka kambi mkoani Katavi na kuwezesha kufanya upasuaji kwa wanawake wenye matatizo ya fistula mkoani humo. Lengo ni kuwafikia akina mama wengi zaidi nchi nzima.

Dkt Gwajima amewapongeza wataalamu hao kwa moyo wa uzalendo na amewahakikishia kupata ushirikiano wote Ili wapanue huduma yao na kuwafikia wananchi wengi zaidi.