April 25, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Rais Samia apokea hati za utambulisho kutoka kwa mabalozi wanne

Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akipokea Ujumbe Maalum kutoka kwa Rais Evariste Ndayishimiye wa Burundi uliowasilishwa na Mjumbe maalum ambae pia ni Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki, Vijana, Michezo na Utamaduni Balozi Ezechiel Nibigira, mara baada ya kuwasili Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 14 Januari, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Balozi wa Saudi Arabia hapa nchini Abdalla Ali M. Alsheryan, mara baada ya kuwasilisha Hati yake ya Utambulisho leo tarehe 14 Januari, 2022 Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akipokea Hati ya Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Jamhuri ya Korea hapa nchini Kim Sun Pyo leo tarehe 14 Januari, 2022 Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Indonesia hapa nchini Triyogo Jatmiko leo tarehe 14 Januari, 2022 Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akiagana na Balozi wa Indonesia hapa nchini Triyogo Jatmiko mara baada ya mazungumzo leo tarehe 14 Januari, 2022 Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akipokea Hati ya Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Morocco hapa nchini Zakaria El Goumiri leo tarehe 14 Januari, 2022 Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Balozi wa Morocco hapa nchini Zakaria El Goumiri, mara baada ya kuwasilisha Hati ya Utambulisho leo tarehe 14 Januari, 2022 Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma