May 17, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere (aliyekaa kulia), akisaidiwa kuangalia michango yake katika Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) na Kaimu Meneja Uhusiano na Elimu kwa Umma PSSSF, Abdul Njaidi (wapili kushoto) na Afisa Matekeleza Mwandamizi wa Mfuko huo, Donald Meeda wakati alipotembelea banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam katika viwanja vya Julius Nyerere maarusu Sabasaba barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

PSSSF yaanzisha mfumo wa huduma kwa wanachama popote wanapokuwa

Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online, Sabasaba

MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umeanzisha mfumo wa kisasa wa kutoa huduma kwa wanachama wake kupitia njia ya mtandao popote wanapkuwa yaani (online portal).

Afisa Matekelezo Mwandamizi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bi. Zainab Ndullah (kushoto) akimuhudumia mwanachama huyu wa Mfuko aliyefika banda la PSSSF viwanja vya Sabasaba Julai 5, 2020

Mfumo huo umeanzishwa na mfuko huo ikiwa ni miaka miwili tangu kuanzishwa kwa mfuko.

Mhandisi wa Mifumo ya Kompyuta (System engineer) wa Mfuko huo, Goodluck Msangi, ameeleza jinsi mfumo huo unavyofanya kazi kwenye Banda la PSSSF lililopo katika Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanayoendelea kwenye Viwanja vya Julius Nyerere Barabara ya Kilwa maarufu kama Sabasaba.

Mhandisi Msangi amesema mfumo huo unawawezesha wanachama na wastaafu kupata taarifa mbalimbali kuhusu mwenendo wa michango na taarifa za malipo ya pensheni ya kila mwezi.

“Kwa wanachama wanaweza kupata taarifa ya mwenendo wa michango yao iliyowasilishwa na mwajiri, mstaafu ataweza kupata taariza za malipo ya pensheni ya mwezi kiasi kilicholipwa benki.

Pia mfumo huo unawezesha mawasiliano ya moja kwa moja kati ya mwanachama au mstaafu na mfuko wakati wowote na mahala popote bila ya muhusika kuhitajika kufika kwenye ofisi za Mfuko.” Amefafanua mhandisi Msangi.

Aidha kupitia mfumo huo endapo mwanachama ana maoni, ushauri au anahitaji ufafanuzi wa jambo lolote anaweza kufanya hivyo na mrejesho atapata mara moja.