Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda, amewataka Vijana nchini kutumia muda vizuri wanapopata nafasi ya kwenda Jeshi la Kujenga Taifa ( JKT).
“Sisi tuliopita JKT miaka ya zamani huko, hatuna budi kuwaambia vijana wa leo kwamba tumieni muda huu vizuri mnapopata nafasi ya kwenda JKT, JKT ambayo sasa inalenga kuwaimarisha vijana na kuwapa uwezo wa kuweza kuanza maisha yao wenyewe kutokana na ujuzi walioupata kutoka maeneo ya makambi ya JKT”
Mhe. Pinda ameyasema hayo Agosti 6,2026 wakati alipotembelea Banda la JKT katika Maonesho ya Wakulima (Nanenane), yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Malecela, Nzuguni Dodoma.
Amefafanua kuwa JKT ni shule nzuri kwa vijana, kwani limetengeneza utaratibu mzuri wa kuwapa mafunzo vijana hususani katika suala zima la ubunifu. Vijana wanafundishwa ubunifu wa kutengeneza vitu mbalimbali ambavyo vinaweza kuwasaidia kujikwamua kiuchumi.

More Stories
Nanauka apongeza Kariakoo Kwa kuwezesha vijana Kibiashara
Uzalishaji mbegu bora waongezeka kwa asilimia 55 nchini
Waziri Sangu apongeza ushiriki wa Yas Maonesho Nanenane Lindi