Straika mpya wa Gwambina FC Paul Nonga ilimlazimu arudishe nauli kwa mabosi wa Namungo ambao walikuwa wanahitaji saini yake.
Nyota huyo aliyekuwa Lipuli, alikuwa anahitajika kwenda kusaini Namungo kabla ya Gwambina FC kumvutia kasi na kumpa mkataba.
Nonga amesema kuwa awali alikuwa kwenye mazungumzo na Namungo iliyokuwa na nia ya kupata huduma yake, lakini alibadili maamuzi baada ya Gwambina kumfuata rasmi.
“Nilikuwa kwenye hatua za mwisho kujiunga na Namungo ila Gwambina walipoonyesha nia niliwaelewa na nikaenda kusaini, kwa kuwa nilitumiwa nauli na Namungo ilinibidi niwarudishie mkwanja wao,” alisema Nonga

More Stories
Wajinyakulia zawadi Kampeni ya ‘Vuna na Mixx’
Ajishindia Mil. 50 ‘Kila muamala bao la ushindi’
Watanzania zaidi ya 90 wanufaika ‘ ikiingia tu goli’