Na Mwandishi wetu,Timesmajira
MWANASHERIA Harrieth Ndege ameeleza namna alivyoguswa kwa kina na hotuba ya Makamu wa Rais Dkt. Emmanuel Nchimbi, hasa katika masuala yanayohusu haki, ustawi na maendeleo ya wanawake nchini.
Kutokana na msukumo huo, Harrieth ameungana na Mwanaharakati mzawa Alphonce Muyinga katika juhudi za kujitolea kwa jamii, ambapo walifika katika Shule ya Msingi Michese, Dodoma, kutoa msaada na hamasa kwa wanafunzi.

Aidha, Harrieth amebainisha kuwa miongoni mwa viongozi wanaomvutia kwa utendaji kazi wao ni Dorothy Gwajima, akieleza kuvutiwa na jitihada zake katika kulinda na kutetea haki za mtoto wa kike.
Katika kuonesha kwa vitendo dhamira yake ya kusaidia jamii, Harrieth ametoa msaada wa taulo za kike (sanitary pads), toilet paper na sabuni, ili kusaidia watoto wa kike kujisitiri na kuzingatia usafi wa mwili, hatua inayochangia kuboresha afya na kujiamini kwa wanafunzi hao wakiwa shuleni.

More Stories
Serikali yapongezwa uwekezaji mkubwa wa Kituo cha Kufua Umeme JNHPP
Airtel  yaimarisha mawasiliano vijiji Vitatu
DCB yazindua Kampeni ya ‘Tuma Bure, Shinda Kila Wiki’