Esther Macha, TimesMajira Online, Kyela
MPIGAMPICHA maarufu Jijini Mbeya, Obadia Mwakibinga amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea Ubunge Jimbo la Kyela.
Mwakibinga amesema nia ya kuomba kuteuliwa ni kusaidiana na wananchi wa Kyela kuleta maendeleo.
Aidha amesema changamoto zaJjimbo la Kyela ni pamoja afya, maji, miundo mbinu ya barabara maeneo ya vijijini ni changamoto kubwa.
Akimkabidhi fomu ya kugombea Ubunge, Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Kyela, Lucas Nyanda amewataka wagombea kufuata kanuni na taratibu za chama ikiwa ni pamoja na kuacha tabia ya kujipitisha kwa wapiga kura kabla ya kampeni kuanza.
More Stories
Mbunge ahoji ukamilishwaji miundombinu Vituo vya afya
Mbogo aomba Tume kuchunguza madai ya waliokuwa wafanyakazi wa EAC
Dkt.Mabula aomba mabonde Ilemela yatumike kwa Kilimo cha umwagiliaji