May 4, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Mkuu wa Wilaya :Sijaridhishwa ukusanyaji mapato Mpwapwa

Na Stephen Noel – Mpwapwa.

Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa  mkoani Dodoma ,Sophia Kizigo amesema hajaridhishwa na ukusanyaji wa mapato katika halmashauri  hiyo hali aliyosema inatishia uendelevu wa miradi ya  maendeleo inayoibuliwa na wananchi ngazi za vijiji na kata.

Kizigo ameyasema    halmashauri hiyo ikiwa katika robo ya pili ya  mwaka wa fedha 2022/2023 wamefanikiwa  kukusanya mapato kwa asilimia 41.2% kitu alichosema kinaweza  kutishia halmashauri kushidwa kufikia lengo la ukusanyaji wa mapato katika  halmasahauri hiyo.

Aidha akianisha sababu za halmashauri hiyo kuendelea kusuasua  katika ukusanyaji ni usimamizi mbovu  wa mapato, lakini uzembe wa kusimamia mapato na  baadhi ya  vyanzo kama   madini ya ujenzi ikiwemo vifusi vya kujengea barabara na  miundo mbinu mingine  na kuwatumia watu  ambao si wataalamu wa uchumi katika kukusanya mapato.

Amesema ili kufanikisha hilo lazima watendaji wa kata   vijiji  pamoja na madiwani washirikiane katika kusimamia na vyanzo vya mapato  na kuviwasilisha kwa mamalaka husika.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mpwapwa ambae amebobea katika usimamizi wa fedha,  George Nathan Malima amedai kuwa   kuna uzembe mkubwa unaofanya na mawakala wa ukusanyaji mapato ambapo wakikusanya  hawawasilishi fedha benki hiyo kukaa na fedha majumbani kitu alichokisema kuwa kinaweza kikawa  kinachangia kuto kufikia lengo.

 ‘’Kiukweli ni uzembe wa hali ya  juu pesa inakusanywa haipelekwi benki  lakini pia   kunapesa zinatumika pesa mbichi bila kufuata utaratibu kwa maelekezo ya wakuu wa idarakitu ambacho si kizuri sana katika uhasibu’’ Ameongea.

Baadhi ya Madiwani wakifuatilia mjadala Katika Kikao cha Baraza la Madiwani Mpwapwa

Diwani wa kata ya  berege ambae ni mjumbe wa kamati ya uchumi mipango na fedha ,Baraka Habari amesema  mapato mengi ya halmasahauri  hiyo yanavuja   sana kwa kukosa usimamizi madhubutu.

“Kwa mafano si kwamba mapato hayakusanyi hapana mapato yanakausanaya ila mawakala na watendeji wa kata  hawapeleki fedha hizo Benki wa wakati na mapato mengi yanavuja mfano tumefanya ambushi ya mapato  katika mnada wa Chipogolo  ambapo timu pekee ilikuwa inawasilisha  shilingi million 4 lakin baada ya madiwani  kuungana na   madiwani wameweza kukusanya  hadi million sita ndipo tulipobaini kuwa  mapato ya halamasahauri yanaliwa kwa kukosa usimamizi mathubuti” ameongea.