Mwalmu akiwa amevalia barakoa huku akikagua daftari la mmoja wa wanafunzi katika Shule ya Sangharsh Vidya Kendra iliyopo katika kitongoji cha makazi duni mjini Jammu, India juzi (Picha na AP). Wakazi wakiendelea na pilikapilika huku wengine wakioga na kuchota maji katika Kijiji cha Rodriguez jimboni Rizan, Ufilipino. Kijiji hicho kiliharibiwa vibaya na kimbunga Vamco juzi. (Picha na Reuters). Wafanyakazi wa manispaa wakishirikiana kuweka mti wa Krismasi eneo la Red Square ambalo lina makumbusho ya kihistoria kushoto na ofisi za Jimbo la Gum kulia. Tukio hilo lilifanyika jana mjini Moscow nchini Urusi ikiwa ni maandalizi ya sikukuu za Krisimasi na Mwaka Mpya. (Picha na AP). Mwanamke raia wa Palestina akiwa amesimama na watoto wake mbele ya nyumba yao iliyopo katika makazi duni Kusini mwa Ukanda wa Gaza juzi. (Picha na AP). Maafisa wa Jeshi la Polisi wakiwa wamejipumzisha huku wakitumia simu zao karibu na eneo la jumba la mfalme mjini Bangkok, Thailand wakati wakiendelea na operesheni ya kudhibiti maandamano ya raia dhidi ya Mfalme Maha Vajiralongkorn wakishinikiza mali za ufalme huo zirudishwe chini ya utawala wa raia. (Picha na Reuters). Maafisa wa Jeshi la Polisi wakiwa wamewaweka chini ya ulinzi wahamiaji kutoka Morocco baada ya kuwasili katika Pwani ya Kisiwa cha Canary nchini Uhispania juzi. (Picha na AP). Post Views: 993 Continue Reading Previous Matukio yaliyosisimua katika pichaNext MATUKIO YALIYOSISIMUA More Stories 1 min read CHAGUO LA MHARIRI (PICHA) Mwenyekiti ACT-Wazalendo akutana na viongozi wa chama hicho taifa March 8, 2024 Judith Ferdnand 1 min read CHAGUO LA MHARIRI (PICHA) Othman ashiriki kikao kamati kuu ACT-Wazalendo March 3, 2024 Judith Ferdnand 2 min read CHAGUO LA MHARIRI (PICHA) Habari Azaki zaungana kutoa msimamo wa pamoja katika mkutano wa COP27 November 2, 2022 Penina Malundo
More Stories
Mwenyekiti ACT-Wazalendo akutana na viongozi wa chama hicho taifa
Othman ashiriki kikao kamati kuu ACT-Wazalendo
Azaki zaungana kutoa msimamo wa pamoja katika mkutano wa COP27