April 25, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

MATUKIO YALIYOSISIMUA

Barafu ikiwa imezingira magari katika eneo la maegesho lililopo mjini Bakhchisaray, Crimea juzi. (Picha na REUTERS).
Watu wakitembea karibu na makumbusho mjini Washington DC, Marekani juzi huku bendera zikipepea nusu mlingoti ikiwa ni ishara ya kuomboleza vifo vya Wamarekani 500,000 waliofariki kwa virusdi vya Corona. (Picha na REUTERS).
Wanandoa waliojitambulisha kwa jina la Bibi na Bwana Lim wakipatiwa chanjo dhidi ya virusi vya Corona (COVID-19) katika Ukumbi wa Senja-Cashew Community nchini Singapore juzi. Nchi hiyo imetangaza kuwa watu wote wenye umri wa miaka 70 na kuendelea watakuwa wamepatiwa chanjo hiyo ndani ya mwezi Machi, mwaka huu. (Picha na THE STRAITS TIMES/GAVIN FOO).
Kondoo wakiwa wanakatiza katika mitaa ya Llandudno, Wales nchini Uingereza juzi. (Picha na REUTERS).
Kikosi cha uokoaji kikitafuta wachimbaji waliofukiwa katika machimbo waliyokuwa wanachimba kinyume cha sheria yaliyopo Kijiji cha Buranga, Parigi Moutong Regency, Sulawesi jana. Ajali hiyo ilisababishwa na mwamba kuporomoka. (Picha na AFP).