October 6, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Malugu apania kuinua kipato cha Wanaliwale, ajitosa Ubunge

Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online, Dar es Salaam

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Liwale, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Amando James Malugu ambaye ni amechukua fomu ya kuwania kiti hicho.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa fomu katika Ofisi za Chama Cha Mapinduzi (CCM) Malugu amesema lengo kuu ni kushiriki katika kumsaidia Rais Dkt John Magufuli kuleta maendeleo nchini.

Amando amesema atahakikisha atashirikiana na Wana-CCM kusimamia ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika utekelezaji.