Klabu ya KMC imeendelea kujiimarisha baada ya kumnasa aliyekuwa beki wa klabu ya Yanga Andrew Vicent maarufu kwa jina la Dante. Beki huyo mahili aliachana na Yanga baada ya mkataba wake na klabu hiyo kumalizika mwishoni mwa msimu wa 2019-20.
Dante amepata dili la mwaka mmoja kuitumikia klabu hiyo yenye maskani yake mkoani kinondoni jijini Dar es salaam. Dante anategemewa kuwa nguzo muhimu kwa klabu hiyo kutokana na uzoefu wake ndani ya ligi kuu Tanzania bara.

More Stories
Serikali yaeleza mkakati kuendeleza michezo,wenye ulemavu
Kamati ya Bunge Yapokea Taarifa ya AFCON 2027
Yanga yatwaa Ngao ya Jamii ,Simba chali