Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
TIMU ya Mtibwa Sugar imekamilisha usajili wa beki wa kulia Hassan Ramadhan Kessy akitokea Nkana Red Devils ya Zambia.
Huo ni usajili wa tano wa ndani ya Mtibwa msimu ambao wanaboresha kikosi chao kwa ajili ya msimu 2020/2021 baada ya msimu uliomalizi kutokuwa mzuri kwao.
Mtibwa ilifanikiwa kujinusuru kushuka daraja baada ya kushinda mchezo wao wa mwisho dhidi ya Ruvu Shooting na kumaliza msimu wakiwa nafasi ya 14.

More Stories
Yas yaendelea kuunga mkono Selous Marathon
Mwinjuma aongoza maelfu washiriki mbio TCB Selous Marathon
Mabalozi wasafiri kwa SGR kushiriki Grand Bunge Bonanza