Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online
TIMU ya Mtibwa Sugar imekamilisha usajili wa beki wa kulia Hassan Ramadhan Kessy akitokea Nkana Red Devils ya Zambia.
Huo ni usajili wa tano wa ndani ya Mtibwa msimu ambao wanaboresha kikosi chao kwa ajili ya msimu 2020/2021 baada ya msimu uliomalizi kutokuwa mzuri kwao.
Mtibwa ilifanikiwa kujinusuru kushuka daraja baada ya kushinda mchezo wao wa mwisho dhidi ya Ruvu Shooting na kumaliza msimu wakiwa nafasi ya 14.

More Stories
Kamati ya Bunge Yapokea Taarifa ya AFCON 2027
Yanga yatwaa Ngao ya Jamii ,Simba chali
Wajinyakulia zawadi Kampeni ya ‘Vuna na Mixx’