May 5, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Katibu Mkuu Dkt. Jingu apongeza hatua za utekelezaji Anwani za makazi Mbeya

Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Dkt. John Jingu amepongeza maendeleo ya utekelezaji wa zoezi la Anwani za Makazi Jijini Mbeya wakati alipokutana na Kamati ya utekelezaji wa zoezi hilo mkoani humo.

Ametoa pongezi hizo wakati alipotembelea na kukagua utekelezaji wa anwani za makazi wakati wa ziara yake ya siku tatu kuanzia tarehe 16 hadi 18 Mei, 2022 mkoani humo.

Aidha alikagua shughuli za uchakataji wa vibao vya nyumba pamoja na nguzo za barabara na mbawa zake vinavyotengenezwa katika karakana ya Allyrich iliyopo eneo la Soweto alielekeza kuongeza kasi ya utengenezaji kwa kushirikiana na Watendaji wa Kata ili kuhakikisha zoezi linakamilika kwa wakati.

Dkt Jingu aliwashauri wakandarasi hao kushirikiana na mhandisi ili kuweza kupunguza gharama za nguzo na zoezi la kazi hiyo kukamilika kwa wakati.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Dkt. John Jingu akikagua moja ya kibao cha anwani za Makazi kilichotengenezwa katika karakana ya Allyrich wakati wa ziara yake ya kukagua zoezi la hilo Jijini Mbeya tarehe 16 Mei, 2022
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Dkt. John Jingu akitoa maelekezo kwa Kamati ya utekelezaji wa Anwazi za Makazi alipotembelea na kukagua maendeleo ya zoezi hilo mara baada ya kujionea shughuli za utengenezaji wa vibao na mbawa za anwani za makazi katika Karakana ya Allyrich Jijini Mbeya.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Dkt. John Jingu pamoja na Kamati ya utekelezaji wa Anwani za Makazi  wakitembelea eneo la Sokomatola lililopo Kata ya Maendeleo Jijini Mbeya ikiwa ni sehemu ya ukaguzi wa anwani za makazi.