Na Agnes Alcardo,Timesmajira Online.
MGOMBEA Udiwani kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Selemani Kaniki, leo amejitokeza katika Ofisi za Kata ya Zingiziwa kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya udiwani kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.
Kaniki amepokelewa na makada pamoja na wafuasi wa CCM waliokuwa wakimsubiri kwa muda mrefu leo.
Tukio hilo lilihudhuriwa pia na viongozi wa chama ngazi ya kata, mashina na wanachama mbalimbali, hali iliyodhihirisha mshikamano wa kijamii katika kumuunga mkono juhudi za CCM.





More Stories
Upatikanaji wa maji Chunya wafikia asilimia 52
MiXX Yakabidhi Zawadi kwa Washindi wa Kampeni ya Kombe la Dunia
Mwenge wazindua jengo lenye thamani ya bil 3.4