May 2, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

DC Ilala awapa kibano wajenzi madarasa sekondari

Na Heri Shaaban


MKUU wa Wilaya ya Ilala Ng’wilabuzu Ludigija amewapa kibano Mafundi waliopewa tenda ya ujenzi wa madarasa ya Shule za Sekondari yanayojengwa kwa fedha kutoka Shirika la Fedha la kimataifa IMF akiwataka ujenzi wa Madarasa hayo ujengwe kwa wakati.

Mkuu wa Wilaya Ludigija alitoa tamko hilo leo katika ziara yake na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya kukagua maendeleo ya madarasa hayo ambayo yanatakiwa yakamilike mwezi Desemba mwaka huu.

“Wakandarasi wote ambao wamepewa tenda katika ujenzi wa shule hizi wapewe fedha zao watumie wafanyakazi wa kutosha madarasa yamalizike kwa haraka ili watoto wetu waweze kusoma January “alisema Ludigija

Katika ziara hiyo Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya wametembelea shule za sekondari za Jimbo la Ilala ,Jimbo la Segerea na Jimbo la Ukonga ambapo kote serikali imepeleka fedha kila kata kwa ajili ya madarasa ili Mwezi January wanafunzi wa kidato cha kwanza wasome

Ludigija alisema jumla ya madarasa 255 ya Sekondari yatarajia kujengwa Wilaya ya Ilala kufuatia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwapatia fedha shilingi bilioni 5.1ambazo zitajenga madarasa 255

“Nampongeza Rais wetu kuwekeza katika sekta ya Elimu ametupatia fedha za kutosha shilingi Bilioni 5.1 kwa ajili ya ujenzi vyumba vya madarasa ujenzi unaendelea vizuri tutasimamia fedha hizi kufanikisha ujenzi wa madarasa 255 “alisema Ludigija

Alisema ziara hiyo ni endelevu kukagua madarasa ya shule za zote za Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam lenye shule 41 jana amefanikiwa kukagua shule nane kati 41 Msimbazi ,Mchikichini na Mivinjeni,Jimbo la Ilala ,Segerea wamekagua kuangalia maendeleo ya ujenzi shule za Magoza Kisukuru na Bonyokwa pamoja na Jimbo la Ukonga .

Mkuu wa Wilaya Ilala Gw’ilabuzu Ludigija akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Ilala leo Novemba 30/2021 katika ziara ya kukagua madarasa ya sekondari ya Fedha kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa IMF , shule ya Mchikichini wakati akiongea na Mafundi (kushoto)Meya wa halmshauri ya jiji Omary Kumbilamoto

Mkuu wa Wilaya Ilala Gw’ilabuzu Ludigija akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Ilala leo Novemba 30/2021 katika ziara ya kukagua madarasa ya sekondari yanayojengwa kwa Fedha kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa IMF ,shule ya Mchikichini