TAARIFA KWA UMMA
*KATIBU MKUU WA CCM ATHIBITISHA KUPOKEA BARUA YA KUJIUZURU KWA SPIKA WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA*
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndg. Daniel G Chongolo leo tarehe 06 Januari, 2022 amethibitisha kupokea barua ya Mhe. Job Yustino Ndugai (Mb) ya kujiuzuru nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katibu Mkuu ameeleza kuwa mchakato wa kumpata Spika mwingine baada ya nafasi hiyo kubaki wazi unaendelea.
Imetolewa na;
Said Said NguyaAfisa Habari Ofisi ya Katibu Mkuu CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)

More Stories
Zambia yapongeza mafanikio ya Tanzania Sekta ya Umeme
Miradi ya elimu kunufaika na Mil. 847
NMB, UNCDF wafungua njia mpya kwa kampuni changa za kidijitali