April 24, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Benki ya NBC yaendesha mafunzo kwa wajasiriamali

Na Mwandishi wetu, TimesMajira Online

Benki ya NBC imeendesha mafunzo ya ujasiriamali na uendeshaji wa biashara kwa wajasiriamali wa Mkoa wa Kilimanjaro kwa ili kuwaongezea ujuzi wa kuendesha biashara zao. Mafunzo. hayo yamefanyika Kiirumbe Social Halls, Mjini Moshi.

Zaidi ya mafunzo hayo, Benki ya NBC pia ilipata fursa ya kuwa wenyeji ya zaidi ya wateja hao 200 kwa ajili ya kupata chakula cha jioni katika Dinner Gala iliyoandaliwa maalum na Benki ya NBC.

Aidha Meneja wa Tawi la Benki ya NBC Moshi, Bw Lazaro Mollel alisema nia kubwa ya kuwapa mafunzo na kuwaalika chakula cha jioni ni dhamira ya benki hiyo kutaka kuwaweka wateja wao karibu zaidi.

Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa Benki ya Taifa ya Biashara Dk Kassim Hussein (watatu kushoto), akikabidhi cheti cha kuhudhuria mafunzo ya uboreshaji wa uwendeshaji Biashara kwa Mteja wa Benki hiyo Procles Visent wakati wa hafla ya mafunzo hayo yalioandaliwa na Benki ya Nbc, Mkoa wa moshi wengine pichani kutoka kushoto ni Mkuu wa Kigengo cha wajasiliamali wa Benki ya Nbc Mussa Mwinyidaho, Mkurugenzi wa Biashara Elvis Ndunguru pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Taifa ya Biashara NBC, Nd Elibariki Masuke
Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya Taifa ya Biashara NBC Elvis Ndunguru (wapili kushoto) akitoa cheti cha kuhudhuria mafunzo ya uboreshaji wa uwendeshaji Biashara kwa Mteja wa Nbc Mkoa wa Moshi Laija Mtenga wakati wa hafla ya mafunzo ya uboreshaji wa uwendeshaji Biashara yaliyotolewa kwa wateja wa NBC Mkoa wa Moshi wengine pichani ni Mkuu wa Kigengo cha wajasiliamali wa Benki hiyo Mussa Mwinyidaho, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa NBC Dk Kassim pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Taifa ya Biashara NBC, Nd Elibariki Masuke.
Maofisa kutoka Benki ya NBC na uongozi wa mkoa wa Moshi wakiwa katika picha ya pamoja na Wahitimu wa mafunzo ya uboreshaji wa uwendeshaji Biashara yaliyotolewa na Benki ya Biashara NBC