*Songambele ni mmoja wa wapigania Uhuru wa Tanganyika
*Mmoja wa waasisi wa TANU,CCM
Na Agnes Alcardo, Timesmajira Online.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi hivi punde amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Songea, mkoani Ruvuma na kupokelewa na viongozi wa chama na Serikali mkoani humo, wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed na Katibu wa CCM Mkoa wa Ruvuma, Mohamed Ali Khalfan, leo Juni 2, 2025.
Balozi Nchimbi amewasili mjini Songea, kwa ajili ya kushiriki mazishi ya mwanasiasa mkongwe na mmoja wa wapigania uhuru wa Tanganyika, na waasisi wa Chama cha TANU na CCM, Alhaj Mustafa Songambele, aliyefariki usiku wa kuamkia Juni 1, 2025 jijini Dar es Salaam na kutarajiwa kuzikwa leo mkono humo.

More Stories
Watanzania wahimizwa kudumisha maadili
Elimu ulinzi shirikishi yapunguza mauaji Kwimba
AIRTEL FURSA LAB yarudi kwa sura mpya