MILWAUKEE, Washington
NYOTA wa kikapu katika timu ya Milwaukee Bucks, Giannis Antetokounmpo ameisaidia timu yake kuibuka na ushindi katika mchezo wa fainali game ya 3, Ligi Kuu ya Kikapu nchini Marekani NBA uliofanyika mwishoni mwa wiki huko Milwaukee.
Katika mchezo huo, Antetokounmpo aliifungia timu yake alama 41 na kuwafanya Bucke kuibuka na ushindi wa vikapu 120-100 dhidi ya Phoenix
Suns katika Mchezo 3. Hata hivyo Suns wanaongoza
2-1, na Mchezo 4 utafanyika kesho.
Akizungumza mara baada ya mchezo huo kumalizika kocha wa Suns Monty Williams amesema, robo ya pili na ya tatu kikosi chake hakikucheza vizuri.
Hata hivyo, Suns ilikuwa na wachezaji watano katika takwimu mbili, wakiongozwa na
Pointi 19 za Chris Paul. Deandre Ayton alikuwa na alama 18 na
rebound tisa. Jae Crowder pia alikuwa na alama 18.
%%%%%%%%%%%%%%%%
More Stories
Waziri Mkuu ataka Mbeya Tulia Marathon kuongeza wigo
Tigo washiriki Tulia Marathon 2024
Ramadhani Brothers wafikisha Tuzo ya AGT Mbuga ya Serengeti