May 18, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Wahudumu wa afya wakimpeleka mgonjwa katika Kitengo cha Dharura kilichopo Kituo cha Afya Maimonides,Brooklyn mjini New York,Marekani. (Picha na Andrew Kelly/Reuters).

Watafiti wasema Wamarekani 145,000 watakufa kwa Corona

Na Mwandishi Wetu, TimesMajira Online

Utafiti wa Chuo Kikuu cha Washington, Marekani umebainisha kuwa, idadi ya watu watakaofariki kwa maambukizi ya virusi vya corona (COVID-19) hadi kufikia mwezi Agosti, mwaka huu itakuwa zaidi ya 145,000 nchini humo.

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyoripotiwa na Shirika la Habari la Reuters kupitia ripoti ya watafiti katika Chuo Kikuu cha Washington nchini Marekani.

Kwa mujibu wa watafiti hao, idadi ya vifo hivyo huenda ikaongezeka zaidi kutokana na maambukizi ya virusi vya corona.

Aidha, Taasisi ya Tathmini ya Afya ya chuo hicho cha Washington Ijumaa iliyopita pia ilitabiri kuwa idadi ya watu watakaofariki nchini Marekani hadi kufikia mwezi Agosti, mwaka huu itafikia 140,496.

Tabiri zote hizo zimetolewa huku takwimu zilizotolewa na tovuti ya Worldometers zikionyesha kuwa, watu 113,061 watafariki kwa maambukizi ya corona nchini Marekani kati ya jumla ya watu milioni 2,260,597 waliopatwa na ugonjwa huo.