May 3, 2024

Timesmajira

Gazeti Huru La Kila Siku

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa. (Picha na Maktaba).

Wanakijiji wilayani Uvinza wamlilia Waziri Mkuu

Na Grace Gurisha,TimesMajira Online

WAKAZI sita wa Kijiji cha Mpeta, Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma wamemuomba Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa awasaidie walipwe fedha zao sh.milioni 15, ambazo ni gharama walizotumia kuleta amani katika kijiji hicho kutoka na mapigano ya askari na wananchi yaliyotokea Oktoba 16 na 17,2015.

Pia, walifanikisha kupatikana kwa silaha mbili za Jeshi la Polisi (bastola na SMG) ambazo zilipotea katika mapigano hayo.

Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam na Gerald Ibrahim maarufu Serikali ambae ni mwakilishi wa wanakijiji hao na ndiye aliyeongoza kupatikana kwa silaha hiyo na kupatikana kwa amani kijijini hapo.

Amesema, baada ya tukio hilo, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Kigoma walikaa kikao ndipo Katibu Tarafa wa Nguruka alimweleza kuwa, amepata taarifa kutoka kwa wananchi kuwa yeye unaweza kusaidia kupatikana kwa hizo silaha, kuzuia ghasia na kuleta amani.

“Nilikubali kufanya kazi hiyo iliyokuwa inagharimu sh.milioni 15 ambayo sijalipwa chochote hadi leo, kazi ilifanyika kubwa nilitawanya vikosi vya vurugu na kufanikiwa kupata silaha zilizopotea.

“Tunamuomba Waziri Mkuu atusaidie tulipwe fedha zetu kwa sababu, tulitumia gharama zetu kufanikisha kuleta amani na kupatikana kwa silaha,”amesema Ibrahim.