Na Grace Gurisha,TimesMajira Online
WAKAZI sita wa Kijiji cha Mpeta, Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma wamemuomba Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa awasaidie walipwe fedha zao sh.milioni 15, ambazo ni gharama walizotumia kuleta amani katika kijiji hicho kutoka na mapigano ya askari na wananchi yaliyotokea Oktoba 16 na 17,2015.
Pia, walifanikisha kupatikana kwa silaha mbili za Jeshi la Polisi (bastola na SMG) ambazo zilipotea katika mapigano hayo.
Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam na Gerald Ibrahim maarufu Serikali ambae ni mwakilishi wa wanakijiji hao na ndiye aliyeongoza kupatikana kwa silaha hiyo na kupatikana kwa amani kijijini hapo.
Amesema, baada ya tukio hilo, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Kigoma walikaa kikao ndipo Katibu Tarafa wa Nguruka alimweleza kuwa, amepata taarifa kutoka kwa wananchi kuwa yeye unaweza kusaidia kupatikana kwa hizo silaha, kuzuia ghasia na kuleta amani.
More Stories
Mbunge ahoji utekelezwaji wa ahadi za viongozi majimboni
Rais Samia alivyotunukiwa tuzo ya uchumi Uturuki, azidi kutwaa tuzo za kimataifa
Habari picha: Mbunge wa Malinyi uso kwa uso na Waziri Mkuu Bungeni